PENZI LA MTOTO WA SHANGAZI.

PENZI LA MTOTO WA SHANGAZI By theostar Kwa mawasiliano zaidi 0692-794942 0654-105503. SEHEMU YA 19 Ilipoishia sehemu ya kumi na nane (18)............... "naomba unisikilize na unielewe vizuri mke wangu".... "siwezi kukusikiliza wala siwezi kuondoka hapa" (Jenny alichachamaa kutokubaliana na mimi, alichukua begi lake na kurudi nalo chumbani kwake)............... SASA ENDELEA Jenny aliniacha kwenye mduwazo mkubwa sana baada ya kukataa katakata kuondoka pale nyumbani. Akili yangu ilizidi kuchoka, nilijisogeza taratibu mpaka kitandani na kukaa, kisha nikajilaza kichalichali kwa kukikata kitanda nikifikiria cha kufanya baada ya Jenny kukataa kuondoka. Nilinyanyuka pale kitandani na kumfuata Jenny kule chumbani kwake ili kwenda kumbembe...