PENZI LA MTOTO WA SHANGAZI
PENZI LA MTOTO WA SHANGAZI By theostar Kwa mawasiliano zaidi 0692-794942 0654-105503. SEHEMU YA 29 Ilipoishia sehemu ya ishirini na nane (28).................... "hii siyo sumu, ila ni dawa kiboko ya tumbo, hata kama tumbo lako likiwa linauma vipi ila ukitumia hii dawa maumivu yanaisha papo hapo na hutaumwa tena na tumbo" (yule mzee aliipamba ile dawa kwa maneno matamu ya kuisifia, alijimiminia kidogo ile dawa kwenye kiganja cha mkono wake wa kushoto na kuilamba, alifanya hivyo kwa ajili ya kuihakikisha kuwa ile dawa ilikuwa ni salama, kisha alimpatia Jenny ile dawa baada ya yeye kuionja, Jenny aliipokea ile dawa na kuinywa yote). Baada ya muda mfupi kupita, jenny alianza kulia juu ya maumivu makali sana ya tumb...