Posts

MALIPO YA USALITI

Image
                        MALIPO YA USALITI By Theostar Kwa mawasiliano zaidi 0673-779766 0782-589866                  SEHEMU YA 2  Ilipoishia sehemu ya 1 " (Juma alimsindikiza Halieth kwa macho tu yaliyokuwa yamejawa na tamaa ya kutaka kumwona Halieth akiwa anatembea tu kwa jinsi anavyozichezesha nyama za makalio yake)"............... SASA ENDELEA   Majira ya saa mbili na dakika kumi na tano usiku (20:15) Juma aliwasili Suzy's restaurant sehemu ya makutano. Alipofika sehemu husika Juma alitoa simu kwenye mfuko wa suruali yake na kumpigia Halieth, Halieth alipokea simu iliyokuwa ikiita kwa namba mpya "hallow"... "Halieth, unaongea na Juma! Habari yako" (Juma alianza mazungumzo kwa kujitambulisha kwa Halieth kwa sababu alitumia namba mpya).... Mimi nipo salama, hofu kwako tu...  Mimi pia nipo salama... Ni jambo la kumshukuru Mungu! Mimi nipo njiani naelekea mahala tu...

MALIPO YA USALITI

Image
                    MALIPO YA USALITI By Theostar Kwa mawasiliano zaidi 0673779766 0782589866                 SEHEMU YA 1   Juma na Hairath ni wapenzi wanaopendana sana. Mahusiano yao ya kimapenzi yamedumu kwa muda wa mwaka mmoja na nusu bila kuoana.   Juma alikua ni mfanyakazi katika hoteli ya Cate Hotel inayopatikana Kingorwilwa mjini Morogoro. Kitengo chake cha kazi kilikua cha kupokea wageni mbalimbali wanaofika katika hoteli hio. Siku moja Juma akiwa kwenye majukumu yake ya kikazi alitembelewa na mgeni aliyekuwa anafahamiana nae. "Karibu Halieth" (sauti ya Juma ilisikika kumkaribisha mgeni aliyeingia muda huo)... Asante! (mgeni "Halieth" alishukuru baada ya kukaribishwa na kukaa kwenye kiti kimojawapo vilivyoandaliwa kwa ajili ya wageni wanao ingia hotelini hapo, kisha akaendelea kuongea), habari za kazi rafiki yangu.. Mungu anasaidia vema, kazi zinaenda vizuri, sijui kwa upande wako...

PENZI LA MTOTO WA SHANGAZI.

Image
                                                                PENZI LA MTOTO WA SHANGAZI By theostar Kwa mawasiliano zaidi 0692-794942 0654-105503.   SEHEMU YA 32    Ilipoishia sehemu ya thelathini na moja (31)...................  Safari ya kwenda kwa yule mama tulioelekezwa na yule mama ntilie iliishia pale pale kwa yule mzee. Yule mzee alianza kututembeza katika eneo lake lililozunguka nyumba zake huku stori za hapa na pale zikiwa zinaendelea. "Sasa babu, tunaomba tukuache mara moja tu ili tukachukue kilichochetu pale kwenye nyumba ya wageni".... "sawa vijana wangu" (yule mzee alikubaliana na mimi, tuliondoka na kumuacha mzee Jakob akiwa mwenye furaha sana, tulielekea moja kwa moja kule kwenye nyumba ya wageni tayari kwenda kuchukua kilichochetu ili kuhamishia makazi mapya kwa yule mzee).  ...

PENZI LA MTOTO WA SHANGAZI.

Image
                                                            PENZI LA MTOTO WA SHANGAZI By theostar Kwa mawasiliano zaidi 0692-794942 0654-105503.     SEHEMU YA 31    Ilipoishia sehemu ya thelathini (30)...................  mimi naitwa mzee Jakob hivi mnavyoniona ndivyo nilivyo, mke wangu alikufa miaka miwili iliyopita na kwa bahati mbaya hatukuweza kupata mtoto, "pole sana mzee wangu" (nilimdakia tena yule mzee kwa kumpa pole baada ya kusikia kuwa amempoteza mke wake, na aliendelea kuongea), asante sana kijana wangu, pia nataka niwaambie kitu kimoja ambacho kitakuwa ni cha muhimu sana kwenu......................... SASA ENDELEA   "Eheee, tuambie mzee wangu" (nilimuhimiza yule mzee atuambie hicho kitu kwani nilikuwa na shauku kubwa ya kutaka kukijua kuwa ni kitu gani).... (yule mzee alinyamaza kwa dak...

PENZI LA MTOTO WA SHANGAZI.

Image
                                                        PENZI LA MTOTO WA SHANGAZI By theostar Kwa mawasiliano zaidi 0692-794942 0654-105503.    SEHEMU YA 30   Ilipoishia sehemu ya ishirini na tisa (29)...................... "y uko hapo tu mtaa wa nyuma ndugu yangu".... (yule kijana alikuwa kimya kwa dakika chache) "sawa!, panda hapo twende" (yule kijana alilikubali ombi langu na kuniamuru nipande kwenye gari tayari kwenda kumsaidia Jenny kumpeleka hospitalini).   Baada ya kufika pale kwa yule mzee nilipomuacha Jenny nikiwa na usafiri, nilishtuka sana baada ya kumuona Jenny akiwa tayari...................... SASA ENDELEA   Amepona. Kwa hali ile mbaya niliyomuacha nayo Jenny sikuweza kuamini kama nitamkuta katika hali yake ya kawaida, nilimkimbilia na kupiga goti mbele yake "mke wangu, umepona?" (nilimuuliza Je...

PENZI LA MTOTO WA SHANGAZI

Image
                                                                  PENZI LA MTOTO WA SHANGAZI By theostar Kwa mawasiliano zaidi 0692-794942 0654-105503.   SEHEMU YA 29     Ilipoishia sehemu ya ishirini na nane (28)....................  "hii siyo sumu, ila ni dawa kiboko ya tumbo, hata kama tumbo lako likiwa linauma vipi ila ukitumia hii dawa maumivu yanaisha papo hapo na hutaumwa tena na tumbo" (yule mzee aliipamba ile dawa kwa maneno matamu ya kuisifia, alijimiminia kidogo ile dawa kwenye kiganja cha mkono wake wa kushoto na kuilamba, alifanya hivyo kwa ajili ya kuihakikisha kuwa ile dawa ilikuwa ni salama, kisha alimpatia Jenny ile dawa baada ya yeye kuionja, Jenny aliipokea ile dawa na kuinywa yote).    Baada ya muda mfupi kupita, jenny alianza kulia juu ya maumivu makali sana ya tumb...

PENZI LA MTOTO WA SHANGAZI

Image
                                                                                                    PENZI LA MTOTO WA SHANGAZI By theostar Kwa mawasiliano zaidi 0692-794942 0654-105503.   SEHEMU YA 28    Ilipoishia sehemu ya ishirini na saba (27)....................  Baada ya Jenny kumaliza kusukutua pia aliyanywa yale maji, nilikichukua kile kikombe toka kwa Jenny alipomaliza kunywa yale maji na kumpatia yule mzee kile kikombe. "Tunashukuru sana mzee wangu" (nilizidi kutoa shukurani zangu kwa yule mzee huku akiwa anakipokea kile kikombe, na kuingia nacho ndani). Ghafla Jenny alianza kulalamika kuumwa na tumbo baada tu ya kunywa yale maji..................... SASA ENDELEA    "Babu!, babu" (nilimwita ...